Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Jeshi la Sudan leo (Jumanne 20 Mei, 2025) limetangaza kuwa limekamilisha usafishaji wa Khartoum kutoka kwa Vikosi vya Kijeshi vya Radiamali ya Haraka.
Jeshi la Sudan, katika muktadha wa operesheni yake kubwa ya kijeshi iliyozinduliwa wiki chache zilizopita kwa lengo la kurejesha makao makuu ya mwisho ya Vikosi vya Radiamali ya Haraka kusini na magharibi mwa Omdurman, upande wa kingo wa mto kutoka Khartoum, Mji Mkuu wa Sudan, limetangaza kuwa Khartoum imekwisha safishwa kabisa kutoka kwa vikosi hivyo.
Kulingana na Euronews, Nabil Abdullah, msemaji wa jeshi la Sudan, alisema: “Khartoum imekwisha safishwa kabisa kutoka kwa waasi wa Vikosi vya Radiamali ya Haraka vinavyosimamiwa na Mohammed Hamdan Dagalo ‘Hemeti’.Operesheni hii inaendelea kama sehemu ya usafishaji wa kina wa mji mkuu.”
Sudan imeushutumu Umoja wa Falme za Kiarabu kwa kuingilia kati moja kwa moja kijeshi katika mzozo wa nchi hiyo na kuufanya uwajibike na shambulizi la tarehe 4 Mei lililotokea katika mji wa Port Sudan.
Your Comment